Kurasa

Mbunge wa Bunge la FG na Maofisa waliouawa mjini Mugadishu,Al-Shabab yathibitisha kuhusika.



Watu waliokuwa wamejihami na silaha wamemwua Mbunge mmoja katika Bunge la Serikali ya FG kwenye Wilaya ya Hamar Weyne mjini Mugadishu.



Walioshuhudia wanasema katika Wilaya ya Hamar Weyne ameuawa Mbunge mmoja aliyetajwa kwa jina la Mayow na mwanaume mwingine aliyewahi kuwa mbunge wakati wa Utawala wa Sheikh Sharif.



Habari zaidi zinaeleza kuwa watu waliotekeleza mauaji hayo walikuwa na Gari na baada ya kufikia malengo yao waliondoka katika eneo la tukio,Mashuhuda wameleza kuwa Maaskari wawili pia waliauwa kwenye shambulio la Hamar Weyne ambapo mmoja alikuwa ni Afisa mwenye cheo wa Ikulu ya Villa Somalia.


Punde tu baada ya shambulio hilo Harakat Al-Shabab Al Mujahideen ilizungumza na vyombo vya habari na kuthibitisha kuhusika mauaji hayo,Sheikh Abdulaziz Abuu Mus'ab Msemaji wa Kijeshi wa Al-Shabab ameliambia vyombo vya habari kuwa vikosi vyao vilihusika kuwaua maofisa 3 na kumjeruhi vibaya Mbunge mwingine wa Bunge la FG.


Ni siku ya pili ambapo kuna mfululizo wa mashambulio ndani ya mji wa Mugadishu,siku ya jana aliauwa Afisa mwenye cheo cha juu katika kitengo cha Makachero wa Serikali ya FG.


Liban Jehow Abdi

SomaliMemo,Mugadishu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni