Kurasa

Kikosi cha Anga cha Al-Shabab chadungua Ndege ya Kijeshi ya Kenya nje ya mji wa Kismaayo.



Habari kutoka Mkoa wa Jubba zinaeleza kuwa Ndege mmoja aina ya kivita inayomilikiwa na Wanajeshi wa KDF waliofanya uvamizi katika Ardhi ya Somalia imeharibika vibaya.



Mwandishi wa habari aliyopo Mikoa ya Jubba ameliambia SomaliMemo kuwa Ndege ya kivita aina ya MIG imeanguka eneo iliyo na umbali wa KLM 50 kutoka mji wa Kismaayo na Marubani wawili wa ndege hiyo wameuawa.



Afisa mmoja wa Harakat Al-Shabab Al Mujahideen amethibitisha kuwa kikosi chao cha anga wamefanikiwa kudungua ndege ya kivita wakati ambapo ilikuwa ikifanya mashambulio kutoka angani katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Lower Jubba.


Wakaazi wamesema waliona moto ukiwaka eneo iliyoangukia Ndege hiyo ambayo ni eneo linalojulikana Daseg-Wamo ulio umbali wa KLM 50 kwenda mji wa Kismaayo. 



Fuatilia yatakayojiri

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni